Na John Gagarini, Kibaha
WATU wenye ulemavu wa kutoona wilayani Kibaha mkoani Pwani
wameipongeza serikali kwa kutafsiri kwa lugha ya alama sheria mpya ya
ugonjwa wa Ukimwi ya mwaka 2008.
Mratibu wa mradi huo kwa watu wasioona wilayani humo Bw Robert Bundala
alisema kuwa kwa muda mrefu sheria nyingi zilikuwa hazijatafsiriwa kwa
lugha hiyo maarufu kama nukta nundu hali ambayo ilikuwa haiwapi nafasi
ya kujua sheria hizo.
Bw Bundala alisema kuwa kutokujua sheria hizo kulisababisha kushindwa
kujua mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na haki zao za kimsingi.
"Tunaishukuru serikali kwa kutukumbuka kwani sasa watu wasioona
wanaweza kuisoma na kujua kilichomo na kuweza kudai haki zao ambazo
wanastahili katika sheria hiyo ambayo itakuwa ikielezea juu ya namna
ya kukabiliana na ugonjwa huo na kujilinda," alisema Bw Bundala.
Alisema kuwa mbali ya kutafsiriwa kwa lugha yao ambayo imewarahishia
kuielwa pia mwanzo ilikuwa kwa lugha ya Kiingereza lakini kwa sasa
imeandaliwa kwa Kiswahili na imekuja kwa wakati muafaka.
"Watu wasioona walikuwa kwenye wakati mgumu kutokana na maumbile yao
kwani walikuwa hawajui kilichomo wala haki zao kupitia sheria hiyo,"
alisema Bw Bundala.
Mratibu huyo alisema kwa sasa wanafanya mafunzo kwa wanachama zaidi ya
300 pamoja na viongozoi wote kuanzia ngazi ya kata hadi vijiji ili
kuijua waweze kuitekaleza katika ngazi zao.
"Tumewashirikisha viongozi hao pamoja na wale wa kisiasa wakiwemo
madiwani kwani wao ndiyo wanaoandaa mipango mbalimbali kwenye jamii
ili nao waweze kunufaika," alsiema Bw Bundala.
Aliitaka jamii kubadili mwelekeo kwa kuwasaidia ili waweze kujikwamua
na mazingira magumu waliyonayo kutokana na maumbile yao na kutowaona
kama mzigo ndani ya jamii ambapo wao wanauwezo kama wale wasio na
ulemavu.
mwisho.
Monday, February 27, 2012
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment